Tuesday, May 24, 2016

MOHAMED MCHENGERWA (MBUNGE) ATOA GARI KATIKA CHUO CHA MAENDELEO RUFUJI (IKWIRIRI FDC)

Cecilia Mfuko - Ikwiriri FDC
Mkuu wa chuo cha IKWIRIRI FDC mama Cecilia Mfuko amepokea gari moja kutoka kwa Mbunge wa Rufiji Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa.  Gari hilo lilikuwa limeombwa kwa Mbunge huyo katika siku za nyuma na Mbunge alipokea ombi hilo na akakubali kulifanyia kazi. Siku ya jana tarehe 24 May 2016 katika sherehe za kupokea mwenge hapa chuoni, katibu wa Mbunge Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa katika hotuba yake alisema kuwa  Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa ametoa gari moja kwa ajili ya mafunzo ya udereva katika chuo cha IKWIRIRI FDC. 

No comments:

Post a Comment