UGENI WA MKUU WA MKOA WA PWANI – IKWIRIRI FDC
Jana mkuu wa chuo (Cecilia R mfuko),
alipata ugeni kubwa wa Mh Mkuu wa mkoa na Mh Mkuu wa Wilaya. Mkuu wa mkoa
aliahidi kuzifanyia kazi changamoto zinazokikabili chuo chetu kama ifuatavyo.
1. Changamoto ya
mgogogoro wa ardhi, Mh Mkuu wa Mkoa aliagiza Uongozi wa Wilaya ya Rufiji ukae na
uongozi wa kijiji cha Ikwiriri kusini na kushughulikia suala la mgogoro wa
ardhi na liishe mapema kwani limekuwa ni la muda mrefu.
2. Changamoto ya
Computer na Projector, mh. Mkuu wa Mkoa alisema kwamba ataongea na
wawekezaji wa mkoa wa Pwani ili wasaidie kutoa computer na projector hapa
chuoni kwa ajili ya mafunzo kwa wanafunzi.
3.Changamoto ya
majengo chakavu, Mh Mkuu wa mkoa alisema kuwa ataongea na Mh. Waziri
husika ili kumaliza kabisa changamoto hii.
4.Changamoto ya
kozi ya udereva (driving school), Mh Mkuu wa mkoa alifurahi sana kwani
katika mkoa wa pwani na hasa wilaya ya Rufiji kumegubikwa na vijana wanaondesha
bodaboda na magari bila ya leseni ya udereva. Na hivyo amemuagiza OCD
kushirikiana na chuo ili kumaliza kabisa TATIZO HILI, kwani litapunguza ajali
na vifo kwa vijana wetu.
No comments:
Post a Comment